ads

adds

TFF WAGEUKA MBOGO KWA SIMBA,YANGA ,TRANSIT CAMP NA KMC



Shirika la soka nchini Tanzania (TFF) limesimamisha michezo yote ya kirafiki iliyopangwa kuchezwa kabla ya ligi kuu Tanzania Bara kuanza tarehe 13 Juni. TFF wamefikia maauzi hayo baada ya klabu za Simba ,Yanga ,KMC na Transit Camp kucheza mechi za kirafiki bila taarifa rasmi kwa shirikisho hilo.

Kupitia barua ya wazi kutoka shirika hilo imetoa maelekezo kuvitaka vilabu hivyo kukutanishwa pamoja na kupewa onyo kali na kuna uwezekano kukawa hakuna mchezo wowote utakaochezwa mpaka ligi kurejea huku sababu kubwa ni vilabu hivyo kushindwa kufuata kanuni za kujikinga na Covid 19 hususani kwa mashabiki wake.






Post a Comment

0 Comments