advertise with us

ADVERTISE HERE

SEHEMU YA KWANZA: ZIFAHAMU SABABU ZA BUNDESLIGA KUREJEA MAPEMA

Ligi kuu nchi nchini Ujerumani ilirejea mapema zaidi kwa ligi zinazocheza Michuano ya Ligi ya Mabingwa ulaya na kuifanya kukaribia kumalizika kabla ya juni 31 . Nimekuletea sababu zilizopelekea Bundesliga kurejea mapema zaidi 


1.USHINDANI KATIKA LIGI

Ligi kuu nchini Ujerumani ilikuwa ya kwanza kutangazwa kurejeshwa na chama cha soka nchini humo (DFL) .binafsi naona ni jambo la busara kwa klabu hizo kukubali  kumalizia msimu wao wa ligi bila utata . Vilabu vimekubaliana kucheza mechi 9 kwa kila timu ili kumaliza msimamo.Kutokana na ushindani mkubwa baina ya timu hizo ilikuwa ni ngumu kwa DFL kutoa kombe kwa Bayern Munich anayeongoza kwa  point 55 huku anayemfuata ni Borrusia Dortmund akiwa na point 51,nafasi ya tatu ni RB. Leipzig wakiwa na point 50 huku M,glaidbach akiwa na point 49. Ni ngumu sana kwa msimamo kama huu kutoa kombe kwa klabu yeyote .

Ukitazama msimu wa 2018-19 ligi kuu Ujerumani imeonekana kuleta ushindani kuliko misimu michache iliyopita . Bayern Munich alitwaa Bundesliga kwa tofauti ya point 2 dhidi ya hasimu wake B.Dortmund  huku akipishana kwa point 12  na aliye nafasi ya tatu RB.Leipzg .

Ushindani huu umeongeza ufuatiliwaji wa BundesLiga duniani kote baada ya kufanya vizuri kwa vilabu vyake kwenye michuano ya ligi ya mabingwa ulaya .

2. MAPATO NDANI YA BUNDESLIGA

Ligi ya Ujerumani ni tofauti kabisa na ligi nyingine linapokuja suala la ukusanyaji mapato. Wakati ligi mbali mbali zikijipatia faida kwa kuuza tiketi za mechi kwa Bundesliga ni asilimia 14.1 tu ya mapato yanatokana na viingilio.

Bundesliga inategemea zaidi Uuzaji na ununuzi wa wachezaji ambao huingiza asilimia 16.9 ya mapato, Matangazo ya viwanjani asilimia 22.9  ya mapato huku asilimia 46.1 wakipata kupitia mikataba na vituo virushavyo mechi hizo.

Mwaka 2008 BundesLiga ilikuwa na mapato ya Euro bilioni 1.7 huku mwaka 2019 ilikuwa na mapato ya Euro bilioni 4.019 .

Na mwaka 2019 waliweka rekodi kwa kupata Euro Bilion 1.25 kupitia matangazo ya urushaji wa televisheni

Kwa takwimu hizo unaweza kusema BundesLiga inaweza kuchezwa bila mashabiki na ikapata faida pasipo hasara.

ITAENDELEA KESHO

Post a Comment

0 Comments