advertise with us

ADVERTISE HERE

RATIBA MPYA YA UEFA CHAMPIONS LEAGUE HII HAPA

Shirikisho la soka barani Ulaya ( UEFA ) limethibitisha kuwa mashindano ya ligi ya mabingwa ulaya yatachezwa kwa muda wa siku 12 jijini Lisbon, UrenoTimu 8 zilizobaki katika mashindano hayo zitacheza mechi kwa njia ya mtoano kuanzia hatua ya robo fainali kuanzia Agosti 12 mpaka 23


Timu 4 ambazo bado hazijafuzu hatua ya robo fainali zikiwemo Manchester City na Real Madrid kutoka hatua ya 16 bora zitamalizia mechi zao tarehe 7 na 8 Agosti 2020.

UEFA bado hawajaamua hizo mechi za hatua ya 16 zilizobaki kama zitachezwa kwenye viwanja vya wenyeji ( kama Etihad ) au zitapigwa Ureno pia.Wakati huo huo mechi za Europa League kuanzia hatua ya robo fainali nazo zitapigwa katika viwanja vinne nchini Ujerumani kuanzia Agosti 10 mpaka 21.


Ratiba ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE MSIMU WA 2020/21


Post a Comment

0 Comments