TETESI ZA SOKA DUNIANI LEO JUMATATU TAREHE 06-04-2020

Mshambuliaji wa Borussia Dortmund na timu ya taifa ya England Jadon Sancho, 20, amekataa uhamisho wa kuelekea Manchester United mwisho wa msimu huu iwapo watashindwa kufuzu katika michuano ya klabu bingwa (Sun)
Real Madrid inataka kumsaini mshambuliaji wa Tottenham na England Harry Kane mwenye umri wa miaka 26. (Sport)
Leicester, Newcastle, Crystal Palace na Aston Villa wana hamu ya kumsajili mshambuliaji wa Rangers na Colombia Alfredo Morelos, 23. (Talksport)
West Ham imekuwa ikiwasiliana na wakala wa mshambuliaji wa Chile Alexis Sanchez huku wakifikiria kumsaini mshambuliaji huyo wa zamani wa Arsenal na Manchester United .
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 kwa sasa anahudumu kwa mkopo katika klabu ya Inter Milan kutoka Man United. (Sport Witness)
Kiungo wa kati wa Manchester City na Uhispania David Silva, 34, huenda akapatiwa mechi ya mwisho ya kumuaga katika uwanja wa Etihad mwisho wa msimu iwapo mlipuko wa coronavirus utamzuia kuwaaga mashabiki wa klabu hiyo baada ya kuichezea klabu hiyo kwa miaka 10 kitu ambacho kimemsaidia kushinda taji la ligi kuu mara. (Mail)
David SilvaHaki miliki ya pichaS
Aliyekuwa mshambuiaji wa Manchester United na Tottenham Dimitar Berbatov anaamini kwamba mshambuliaji wa klabu ya RB Leipzig na Ujerumani Timo Werner, 24, atafurahia kujiunga na Bayern Munich badala ya Liverpool mwisho wa msimu huu . (Mirror)
Leicester, Tottenham na Everton wote wana hamu ya kumnunua kiungo wa kati wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 25 Baptiste Santamaria, ambaye anaichezea klabu ya Angers katika ligi ya daraja la kwanza ya Ufaransa. (Express)
Klabu za ligi ya Premia zimenunua vifaa vyao vya kupima virusi vya corona huku kukiwa na hofu kwamba mechi zitachezwa bila mashabiki. (Star)
Beki wa Uholanzi na Manchester United Timothy Fosu-Mensah, 22, anakabiliwa na hali ya switofahamu katika klabu hiyo huku mkufunzi Ole Gunnar Solskjaer akifikiria iwapo anaweza kumuongezea mwaka mmoja katika kandarasi yake (Mirror)
Fosu Mensah
Mshambuliajhi wa Celta Vigo na Urusi Fedor Smolov, 30, alikiuka hatua ya Uhispania kuweka sheria ya kutotoka ndani , akiwa ni mchezaji wa pili wa taifa hilo kwenda kinyume na sheria hiyo kwa kurudi nchini mwake. (AS, in Spanish)

Post a Comment

0 Comments