TAARIFA MUHIMU KWA MASHABIKI WA SIMBA SC



Tunapenda Kutoa Taarifa kwa Wapenzi, Mashabiki na Wanachama wote waliopo kwenye Group mbalimbali za Simba kuwa Waweze kutumia utaratibu wa kutambuzi wa mwanzo ndani ya group kwa kuanza kutoa majina ya Wanachama wenye kadi za Simba na wale ambao hawana kadi kwa maana sio Wanachama bali ni Mashabiki.

Kwa maana hii tutaweza kujuana kuwa nani ni nani na anahitajika nini afanye kwa wakati gani.

MFANO MUHIMU
Kwa wote ambao ni mashabiki ni lazima waanze kwenda kuchukua Kadi za mashabiki Equity Bank au kuanza kujiorodhesha matawini sehemu walipo ambako huduma ya Equity bank haijafika ili kuweza kuwatambua na kufikiwa kwa huduma.

MWISHO

Hatutaruhusu hapo baadae kuwepo watu kwenye group za Simba zilizosajiliwa kama wewe sio Mwanachama hai au Mshabiki wenye kadi ya Equity.Lazima tubadilike tuwe Rasmi tuipende Simba kwa vitendo.


Post a Comment

0 Comments