BETI NASI UTAJIRIKE

TETESI ZA SOKA DUNIANI LEO JUMANNE TAREHE 03-03-2020

Kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba, 26, atarejea katika mazoezi ya kikosi cha kwanza Manchester United wiki hii na anapania kubuni ushirikiano uwanjani na Bruno Fernandes aliyejiunga na klabu hiyo Januari. (ESPN)
Manchester United wanaongoza katika kinyang'anyiro cha kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Muingereza Jadon Sancho, 19, kwa bei inayotarajiwa kuvunja usajili wa katika ligi kuu ya Premia msimu wa joto. (Telegraph)
United pia inajiandaa kumenyana na Liverpool kupata saini ya Sancho kwa £100m, pamoja na mshambuliaji wa RB Leipzig wa miaka 23-Mjerumani Timo Werner. (Express)
Jadon SanchoHaki miliki ya picha
Real Madrid na Paris St-Germain pia wanamnyatia Sancho, ambaye anataka kurejea England. (Mirror)
Huku hayo yajijiri, Werner amejiondoa kwenye mtandao wa Twitter wa klabu yake ya sasa Leipzig baada ya wao kutumia picha yake akijibu maswali kuhusu Liverpool kushindwa kwa mara ya kwanza katika msimu huu wa ligi ya Premia. (Echo)
Leipzig Timo WernerHaki miliki ya picha
Mkufunzi wa Leipzig Julian Nagelsmann hangelipendelea kumuachilia beki wa Manchester City Angelino,23, ambaye kwa sasa anachezea klabu kwa mkopo - lakini anasema bei ya Mhispania huyo ni "ni ghali mno" na kwamba huenda akawa vigumu kumpatia mkataba . (Kicker - in German)
Beki wa Muingereza Mason Holgate, 23, anasema lengo lake ni kujiunga na Everton licha ya klabu nyingine kama Manchester City kuonesha nia ya kutaka kumnunua. (Mail)
AngelinoHaki miliki ya picha
Wasaka vipaji wa Everton' wapo Italia "kutathmini" uwezekano wa uhamisho wa winga wa Napoli na Mexico Hirving Lozano, 24. (Area Napoli, via Star)
Leicester wanamfuatilia beki wa Burnley Muingereza Charlie Taylor, 26, anayepigiwa upatu kuchukua nafasi ya kiungo wa kimataifa wa England Ben Chilwell, 23. (Times)
Mkufunzi wa Chelsea Frank Lampard anaamini kipa wa klabu hiyo Mhispania Kepa Arrizabalaga, 25, bado anastahili kupewa nafasi katika klabu hiyo. (Mail)
Kepa Arrizabalaga
Beki wa Brazil Alex Telles, 27, amabaye ananyatiwa na Chelsea, amekataa ombio la kurefusha mkataba Porto. (A Bola, via Sun)
Mkufunzi wa Arsenal Mikel Arteta anahofia klabu hiyo isipofuzu kwa Champions League msimu huu itakuwa na wakati mgumu kuwavutia wachezaji. (ESPN)

Post a Comment

0 Comments