BETI NASI UTAJIRIKE

KELVIN YONDANI AMGOMEA TENA KOCHA EYMAEL



Kocha Mkuu wa Yanga Luc Eymael alitoa mapendekezo wachezaji waliokosa safari ya mkoani Lindi wajieleze kwa nini wasichukuliwe hatua za kinidhamu.Ni mapendekezo ambayo yalibarikiwa na uongozi  wa Yanga kwenye kikao walichokutana na Mbelgiji huyo hivi karibuni

Nyota takribani saba wakiongozwa na David Molinga, waliingia kwenye mtego huo wa kutakiwa kutoa maelezo.Kelvin Yondani, Lamine Moro, Erick Kabamba, Haruna Niyonzima, Mohammed Issa 'Banka' na Abdulaziz Makame 'Bui' ni miongoni mwa waliokosa safari hiyo

Yondani aweka ngumu

Wakati wachezaji wengine wakiwasilisha utetezi wao Makao Makuu, imeelezwa mkongwe Kelvin Yondani amegoma zoezi hilo

Yondani amesema yeye aliomba ruhusa mapema kuwa alikabiliwa na matatizo ya kifamilia na uongozi ulimkubalia.Hivyo hakubaliani na suala la kutakiwa kujieleza  tena wakati taarifa yake iko Makao Makuu

Post a Comment

0 Comments