ads

adds

SIMBA: TUKIWAPIGA AZAM NA YANGA TUKABIDHIWE KOMBE LETU

Jumapili March mosi, mabingwa wa nchi Simba watashuka kwenye uwanja wa Taifa kuikabili KMC katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom


Siku tatu baadae yaani March 04, Simba itarejea Taifa kuikabili Azam Fc kisha kumalizana na Yanga March 08
Kimahesabu, mechi dhidi ya Azam Fc na Yanga zinaweza kuihakikishia Simba ubingwa wa tatu mfululizo
Vinara hao wa ligi wanaongoza ligi wakiwa na alama 62 ambazo ni tofauti ya alama 17 dhidi ya Azam na alama 21 dhidi ya Yanga yenye mechi mbili za viporo
Ushindi katika mechi hizo, utaihakikishia Simba ubingwa kwani tofauti ya pointi itakuwa kubwa zaidi
Lakini pia Azam Fc na Yanga ndio wapinzani wa karibu kwa Simba katika mbio za ubingwa ingawa watahitaji muujiza kuwafikia mabingwa hao watetezi
Simba inaweza kutangaza ubingwa mapema sana kama itashinda mechi hizo wiki ijayo

Post a Comment

0 Comments