BETI NASI UTAJIRIKE

MANCHESTER UNITED YAWEKA REKODI MPYA 2020

Mashabiki wa klabu ya Mananchester United wameendelea kuwa na hali ngumu baada ya timu yao  kuendelea kufanya vibaya kwa mwaka 2020. Tnagu kuanza kwa mwaka 2020 klabu hiyo imecheza michezo mitatu na haijashinda mchezo wowote.


Hii hapa rekodi yenyewe 
 Klabu hiyo yenye maskani yake Carrington ilianza mwaka 2020 kwa kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Arsenal ,Mchezo wa pili ikatoka sare ya bila kufungana dhidi ya Wolves kombe la FA na hapo jana imepigwa mabao  3-1 dhidi ya mahasimu wao Manchester City kwenye mchezo wa nusu fainali kombe la Carabao Cup .mchezo huo uliochezwa dimba la Old Trafford na kuhudhuliwa na watu maarufu akiwemo Wayne Rooney,Paul Scholes na Sir Alex Ferguson. 

Bao la kwanza kwa upande wa Manchester City lilifungwa na Bernaldo Silva dakika ya 17, Bao la pili lilifungwa na Riyad Mahrez dakika ya 33 na Andres Pereira alijifunga bao dakika ya 38. Mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika Manchester City ilikuwa mbele kwa mabao 3-0. Dakika ya 70 Rashford aliipa Manchester United bao la kufutia machozi na mchezo kukamilika kwa manchester city kuingia fainali ya Carabao Cup.


Post a Comment

0 Comments