BETI NASI UTAJIRIKE

SIMBA WATOA TAARIFA RASMI KUHUSU MIRAJI ATHUMAN

Wakati kina Hassan Dilunga wakiendelea kutupia mabao watakavyo kwenye ligi, kwa wiki kadhaa Simba imemkosa Miraji Athumani mmoja wa wafungaji wake bora sana msimu huu kutokana na majeraha


Habari njema ni kuwa Miraji aliyetupia mabao sita mpaka sasa, amepona majeraha na ataanza mazoezi na timu baada ya mabingwa hao wa nchi kurejea leo kutoka jijini Mwanza
Huenda akawa tayari kuwakabili Mwadui Fc kwenye mchezo wa raundi ya nne kombe la Azam (ASFC) ambao utapigwa Jumamos Januari 25 kwenye uwanja wa Uhuru

Kurejea kwake kutaongeza wigo wa watupia nyavu wa Simba wakiongozwa na Meddie Kagere ambaye amefunga mabao 11

Miraji amefunga mabao sita wakati Hassan Dilunga na Deo Kanda wamefunga mabao manne kila mmoja

Post a Comment

0 Comments