Mshambuliaji mpya wa Yanga Bernard Morrison ameanza vyema maisha yake Jangwani baada ya kun'gara kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Singida United
Morrison ameonesha kuwa na vitu vingi mguuni, ana kasi, mbunifu na mchezaji msumbufu kwa mabeki.Morrison ni aina ya mchezaji ambaye Yanga ilikuwa ikimkosa, leo amehusika kwenye mabao mawili yaliyofungwa na Yanga
Kama ameweza kun'gara katika mazingira ya uwanja wa Namfua (LITI), kwa mechi ambazo zitapigwa uwanja wa Uhuru au Taifa, mabeki watakuwa na kazi.Nyota huyo kutoka Ghana anaweza kuwa usajiri bora uliofanywa na Yanga dirisha dogo
0 Comments