SAKATA LA YANGA NA BEKI WAKE KISIKI "DANTE" LAFIKIA PATAMU

Klabu ya Yanga imefanikiwa kushinda kesi yake dhidi ya beki wake kisiki Vicent Andrew maarufu kwa jina la Dante. Klabu hiyo ilikuwa inadaiwa milioni 45 za usajili.


 mchezaji huyo  alifungua kesi kuishtaki klabu ya Yanga  kwa shirikisho la soka Tanzania (TFF) kwa madai ya kudhulumiwa fedha za usajili. Mara baada ya mashauriano ya pande zote mbili mchezaji huyo amelazimika kurejea kikosini Yanga kuendelea na mazoezi kuelekea michezo ijayo ya ligi .

Klabu hiyo kupitia mitandao yake ya kijamii ilimkaribisha tena nyota huyo kwa ujumbe usiokuwa rasmi na uliandika 

"Uongozi wa #MabingwaWaKihostoria🇹🇿Tanzania, unamkaribisha tena kikosini beki @vicentandrew ‘Dante’ baada ya kumalizika kwa shauri la kesi baina ya pande mbili.
Karibu tena Nyumbani"

Post a Comment

0 Comments