BETI NASI UTAJIRIKE

MCHEZAJI MWINGINE AWACHARUKIA VIONGOZI WA YANGA

Viongozi ngazi za juu klabu ya Yanga wanapaswa kujitathmini upya baada ya kushidwa kulipa baadhi ya wachezaji stahiki zao. Imebainika baadhi ya wachezaji hasa wa kimataifa 



wameshaanza kutimka klabuni hapo na inawezekana wasirudi tena nchini kuitumikia klabu hiyo.Mshambuliaji Sadney Urikhob amesema viongozi wengi wa timu hiyo ni wababishaji. Imeelezwa.

Taarifa imesema kuwa Urikhob amekuwa akiwaulizia mara kwa mara juu ya malipo yake na wao wamekuwa wamekuwa wakimpiga kalenda kila siku.

Imeeleza kwa kusema kuwa kila mara mchezaji huyo alipokuwa akikikumbushia kulipwa fedha hizo viongozi wamekuwa si wakweli na ikabidi mpaka afanye maamuzi hayo.

Urikhob ambaye hivi sasa yuko kwao Namibia, amesema mabosi wake wamekuwa wakisema hawana fedha na badala yake wamekuwa wakimweleza aendelee kuwa na subira.

Post a Comment

0 Comments