KLABU YA YANGA YAPATA PIGO JINGINE

Klabu ya Yanga imepata pigo jigine baada ya kuondokewa na mwaachama wake Ibrahim Akilimali maarufu kama mzee Akilimali.  Mzee Akilimali amesumbuliwa na maradhi kwa 



muda mrefu mpaka kufikwa na umauti. Mzee Akilimali aliwahi kuwa katibu wa baraza la wazee Yanga n atakumbukwa kwa misimamo yake. Akilimali amefariki nyumbani kwake Bagamoyo na atasafirishwa kurudishwa makazi yake ya Tandale Dar es salaam.Mazishi yatafanyika kesho saa 10:00 jioni . Amospoti.com inatoa pole kwa Wanayanga na familia nzima ya Mzee Akilimali.

Post a Comment

0 Comments