Hapo jana katibu mkuu wa Yanga DK.David Ruhago alimpokea mshambuliaji Tariq Seif Kiakala akitokea Misri .Dirisha dogo la usajili litafunguliwa tarehe 16 Disemba mpaka 15 Januari
Tariq anatarajiwa kusaini mikataba na mabingwa hao wa kihistoria mara baada ya dirisha dogo kufunguliwa. Mshambuliaji huyo amewahi zitumikia klabu za Biashara United na Stand United kabla ya kutimkia klabu ya Dekernes FC inayoshiriki ligi daraja la pili nchini Misri.
Mshambuliaji huyo anatajwa kuchukua nafasi ya Balinya ambaye amevunja mkataba na kuondoka klabuni hapo .
Rekodi ya Tariq msimu wa 2018/19 akiwa Biashara United
Mchezaji Tariq aliwahi kufikisha magoli matano ndani ya mechi nne alizocheza kwenye ligi kuu Bara
Alifunga dhidi ya Lipuli FC Biashara ikishinda 3-0.
Akafunga dhidi ya Yanga Biashara ikishinda 1-0.
Akafunga dhidi ya Alliance Biashara ikifungwa 2-1.
Akafunga mabao mawili dhidi ya Ruvu shooting Biashara ikishinda 2-0 Ruvu Shooting.
0 Comments