BETI NASI UTAJIRIKE

GRIEZMAN MAMBO BADO MAGUMU BARCELONA HUKU MESSI AKIENDELEZA UFALME WAKE LA LIGA

Mchezaji bora tuzo za FIFA 2019 Lionel Messi ameendelea kuonyesha uwezo wake wa hali ya juu baada ya kufunga bao muhimu dakika ya 86 dhidi ya Manchester  United



Mchezo huo wa La Liga ulipigwa dimba la Wanda Metropolitan na kushuhudiwa na watazamaji 68 huku aliyekuwa nyota wa timu hiyo akirejea dimbani hapo kwa mara ya kwanza toka ajiunge na Barcelona mwezi Septemba 

Kwenye Mchezo huo Griezman alianzia pembeni kama winga wa kushoto na alionekana hana madhara kwa mabeki wa Atletico huku mashabiki wakimzomea na kumtoa mchezoni. Mashabiki hao waliimba "Griezman bora ufe"

Antonio Griezman amecheza michezo 17 ndani ya Barcelona na kufunga mabao 5 pekee tangu kusajiliwa kwake kwa ada ya EURO milioni 120 aitokeaAtletico Madrid.

Lionel Messi anaendelea kuweka rekodi mpya na hapo jana akitimiza mchezo wa 36 dhidi ya Atletico Madrid na kuwafunga mabao 30.  Rekodi nzuri zaidi ni ile  ya Messi dhidi ya Sevilla akifunga mabao 37 kwenye michezo 36 aliyokutana na timu hiyo.

 Barcelona wameendelea kucheza vyema wakichuan vikali na Real Madrid kuelekea ubingwa wa ligi kuu Hispania La Liga huu timu hiz zikilingana pointi baada ya kucheza michezo 14 na kujipatia pointi 31 na kupishana magoli ya kufunga huku Barcelona akiwa na mabao 36 na Real Madrid akiwa na mabao 30.




Post a Comment

0 Comments