Aliyekuwa mshambuliaji wa klabu ya Los Angels Galaxy maarufu kama LA GALAXY ya marekani na amethibitisha kumaliza mkataba na klabu hiyo na sasa anarudi soka la Ulaya
Mchezaji huyo aliyewahi itumikia Manchester United kwa misimu miwili tena kwa mafanikio makubwa amehusishwa kurejea klabuni hapo wakati wa dirisha dogo. Manchester Uited inashida ya mshambuliaji na Ibrahimovic ni chaguo sahihi kwani akiwa hapo aliiwezesha klabu hiyo kutwaa makombo matatu ikiwamo Europa, FA na Super Cup.
Zlatan aliweka picha yake na kuandika " Nilikuja,nikaona na nikafanikiwa . Asante La Galaxy kwa kunifanya niishi tena. Mashabiki wa Galaxy mlimtaka Zlatan,nikawapa Zlatan na mnakaribishwa tena. Sasa rudini mkaangalie BaseBall na stori lazima iendelee "
Mbali na miamba hiyo ya uingereza kumtaka arejee kikosini hapo lakini pia klabu za AC Milan na klabu za China zinatajwa kumwania mchezaji huyo mwenye miaka 38
0 Comments