advertise with us

ADVERTISE HERE

ZLATAN IBRAHIMOVIC AJIWEKA TAYARI KUTUA TIMU HII ULAYA

Aliyekuwa mshambuliaji wa klabu ya Los Angels Galaxy maarufu kama LA GALAXY ya marekani na  amethibitisha kumaliza mkataba na klabu hiyo na sasa anarudi soka la Ulaya



Mchezaji huyo aliyewahi itumikia Manchester United kwa misimu miwili  tena kwa  mafanikio makubwa amehusishwa kurejea klabuni hapo wakati wa dirisha dogo. Manchester Uited inashida ya mshambuliaji na Ibrahimovic ni chaguo sahihi kwani akiwa hapo aliiwezesha klabu hiyo kutwaa makombo matatu ikiwamo Europa, FA na Super Cup.

Zlatan aliweka picha yake na kuandika " Nilikuja,nikaona na nikafanikiwa . Asante La Galaxy kwa kunifanya niishi tena. Mashabiki wa Galaxy mlimtaka Zlatan,nikawapa Zlatan na mnakaribishwa tena. Sasa rudini mkaangalie BaseBall na stori lazima iendelee "

Mbali na miamba hiyo ya uingereza kumtaka arejee kikosini hapo lakini pia klabu za AC Milan na klabu za China zinatajwa kumwania mchezaji huyo mwenye miaka 38



Post a Comment

0 Comments