UJUMBE WA MOHAMMED DEWJI WAIBUA SHANGWE KWA WANASIMBA,SAMATTA ATOA YA MOYONI

Mwenyekiti bodi ya wakurugenzi na mwekezaji wa klabu hiyo Bw. Mohammed Dewji ameibua shangwe kwa mashabiki wa klabu hiyo baada ya kuthibitisha kukamilika kwa 

viwanja vyake vya mazoezi vilivyopo Bunju. Dewji amethibitisha hayo kuptia kurasa zake za mitandao ya kijamii kwa kuandika

"Wala usiumize kichwa katika swala la Bunju. Tayari kimekamilika.Karibuni wote Bunju tarehe 7 Disemba #Nguvu Moja "

Chini ya maandishi hayo aliweka picha za uwanja huo uliokwisha kukamilika na utazinduliwa na raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.DKT John Pombe Magufuli.

Kaili hiyo iliyoendana na picha imeibua hisia za mashabiki wa klabu hiyo na kumsifu pamoja na kumshukuru kwa jambo hilo. huku mchezaji wa Genk na Taifa Staz mbwana Ally Samata akiwa ni mmoja wa waliompongeza Dewji.



Post a Comment

0 Comments