advertise with us

ADVERTISE HERE

UJUMBE HUU WA MO DEWJI UNAMLENGA NANI KATI YA WACHEZAJI NA KOCHA?

Klabu ya Simba hapo jana ilishindwa kutamba mbele ya Prisons Tanzania baada ya mchezo wao uliopigwa dimba la Uhuru- Dar es salaam na  kumalizika kwa sare ya bila kufungana




Mara baada ya matokeo hayo Mo Dewji - Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi klabuni hapo na mwekezaji mwenye asilimia 49 alionekana kutofurahishwa na matokeo hayo hivyo aliweka picha onekanayo hapo juu na kuandika

  "Usitafute ugumu pasipo ugumu! // Don't look for something difficult that has no hardship!" 

Kauli hiyo imeanza kutafsiriwa kama ni ujumbe kwa Kocha na wachezaji wa klabu hiyo. Baadhi ya mashabiki walionekana wakikomenti kwenye peji hiyo kuhoji ujumbe huo unamhusu nani? 
'

Post a Comment

0 Comments