advertise with us

ADVERTISE HERE

TAIFA STARS NA SIMBA ZAPATWA NA PIGO ZITO

Klabu ya Simba SC imepatwa na pigo baada ya lijendari wake Omari Gumbo kufariki hapo jana jioni . Klabu hiyo imeonekana kuguswa  na kusikitishwa na kifo cha mkongwe huyo 



Simba wametumia mitandao ya kijamii kusambaza ujumbe wa kuondokewa na nyota huyo aliyewahi kuitumikia pia timu ya Taifa la Tanzania. Kwenye taarifa hiyo simba waliandika



"Uongozi wa klabu ya Simba SC umepokea kwa masikitiko taarifa za kiungo wa zamani wa kimataifa wa klabu yetu Omari Gumbo ambaye alifariki ghafla jana jioni .

"Gumbo alipata kuwa makamu wa raisi wa klabu chini ya mwenyekiti Hassan Dalali alikuwa namba 6 hodari pia alipata kuichezea Taifa Stars. Tunatoa pole kwa ndugu ,jamaa na familia na watu wote walioguswa na msiba huu"

Mchezaji huyo atazikwa leo jijini Dar es salaam na taarifa kamili tutaitoa hivi karibuni.

Post a Comment

0 Comments