MWAKINYO AMESHAMPIGA TINAMPAY NJE YA UWANJA

Kuelekea pambano la ndondi uzito wa Kati Kati ya mtanzania Mwakinyo na mfilipino litakalopigwa leo hii uwanja wa Uhuru ni kama tayari Mwakinyo ameshashinda

na kinachosubiriwa kwa sasa ni refa kutangaza ushindi kwa bondia huyo mtanzania.hizi ni sababu zinazompa ushindi Mwakinyo siku ya leo ameshashinda nje ya uwanja tayari 

1. Kucheza pambano uwanja wa nyumbani
mwakinyo yupo uwanja wa nyumbani ni sawa na kwamba amekwishashinda mchezo huo. Kawaida mchezo wa masumbwi humfanya bondia aliye nyumbani kushinda kwa urahisi mchezo huo tofauti na bondia mgeni. Mashabiki wamejipanga haswa kumsapoti bondia huyo kwani rekodi zake zinambeba.


2. Bondia Mfilipino aonyesha uwoga kabla ya pambano
Bondia Mfilipino Arnel Tinampay  alionyesha uwoga wake tangu siku ya kwanza alipowasili kwani aliwasili nchini akiwa na mpishi wake hiyo ni dhahiri dalili ya uoga. Tanzania inahoteli nyingi saa za nyota tano na zina wapishi bora ila kuja na mpishi wake kumeibua maswali mengi.

3. Nguvu ya Mashabiki kwenye mchezo huo .
Bondia Timnapay atakuwa na wakati mgumu kwani uwanja wa taifa utajwazwa na shangwe zenye kulitaja jina la Mwakinyo. Ikumbukwe mwakinyo anasapotiwa na vikundi mbalimbali vikiwemo mashabiki wa simba ,Yanga ,Alikiba na Diamond hivyo muunganiko wa vikundi hivi utamfanya Mfilipino kupata wakati mgumu zaidi

Post a Comment

0 Comments