Nahodha wa Taifa Stars na Klabu ya Genk Mbwana Ally Samatta ameendelea kuteka hisia za wadau wa soka duniani na sasa amegeuka stori kwenye vyombo vya habari nchini
Uingereza huku timu kadhaa zikionyesha dhahili kumtaka mshambuliaji huyo.BBC Sport wanasema Newcastle United na West Ham United zinamnyatia mchezaji huyo.
Samatta alipachika bao moja kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Liverpool siku ya Jumanne uliomalizika kwa 2-1 kwa Genk kupoteza.
Mkataba wake una kipengele cha uhamisho chenye thamani ya pauni milioni 10.
Nahodha huyo wa Taifa Stars amefunga magoli sita katika mechi 13 za ligi msimu huu.
0 Comments