advertise with us

ADVERTISE HERE

KOCHA PRISONS AKUBALI MZIKI WA SIMBA, TULIBAHATIKA KUPATA SARE

Klabu ya Prisons Tanzania imeendelea kuwa tisho kwa vigogo wa ligi kuu Tazania baada ya kutopoteza mchezo wowote wa ligi kuu tangu uanze msimu wa 2019/20



Ilitarajiwa Prisons Tanzania ingefungwa kwa mara ya kwanza  na Simba lakini mambo yalikuwa ni tofauti na matarajio ya mashabiki wa Msimbani baada ya timu hiyo kulazimishwa suluhu ya mabao 0-0 na kuifanya Prisons kutopoteza mchezo wowote kwa msimu wa 2019/20 

Baada ya mchezo huo kocha wa Polisi Tanzania alinukuliwa akisema 

"Tumecheza na timu nzuri ,ina uwezo na mipango mizuri na vijana wazuri,ukiangalia timu tuliyocheza nayo ina wachezaji 7 timu ya taifa wakati sisi tunamchezaji 1 tu timu ya Taifa kwahiyo unaweza kuona ubora. Tulikuwa tunacheza na timu ambayo tulipaswa kuchukua tahadhali muda wote wa mchezo, Nidhamu yetu ya kuzuia ilikuwa nzuri sana na imetusaidia kwani pointi 1 kwa gemu kubwa kama hii ni  sawa"

Kwa matokeo hayo Prisons imejikusanyia pointi 16 ikicheza michezo 10 na kuwa nafasi ya 4 kwenye msimamo wa ligi kuu.




Post a Comment

0 Comments