advertise with us

ADVERTISE HERE

WENGER APATA ULAJI MWINGINE FIFA

Kocha wa zamani wa Arsenal, Arsene Wenger amerudi kwenye soka kivingine baada ya kukubali nafasi ya Ukuu katika Idara ya Maendeleo ya Soka ndani ya Shirikisho la Soka duniani FIFA 


Uteuzi huu unaondoa uvumi uliokuwepo kuwa Wenger angejiunga na Bayern Munich kama kocha.
Arsène Wenger aliifundisha klabu ya Arsenal kutoka mwaka 1996 hadi 2019 na sasa wadhifa huo mpya mkubwa utamfanya awe na mamlaka makubwa zaidi upande wa soka duniani.

Wenger ataungana na wajumbe wengine n manguli katika soka kama Diego Maradona na Pele. Uteuzi huo utamfanya wenga kuwa msimamizi mkuu wa masuala ya soka kwa wanaume na wanawake.

Post a Comment

0 Comments