advertise with us

ADVERTISE HERE

YANGA YAWA TIMU YA KWANZA KUPIGWA HAT TRICK

Yanga inakuwa timu ya kwanza kupigwa mabao matatu na mchezaji mmoja "Hat Trick" msimu huu wa 2019/2020.  Mchezaji wa Polisi Tanzania Ditram Nchimbi anakuwa mchezaji wa kwanza kufunga hat trick.


Mshambuliaji huyo alikuwa  mwiba mkali kwa Yanga baada ya kufunga mabao matatu ambayo yangeiangamiza Yanga kama asingekuwepo Moringa basi leo Yanga ingefungwa mabao 3-1.

Ditram Nchimbi alifunga mabao dakika 34,55 na 58 na kuifanya Yanga  kuwa nyuma kwa mabao 3-1.

Ditram Nchimbi si mgeni kwenye ligi kuu Tanzania Bara kwani amevichezea vilabu vya Njombe mji (iliyoshuka daraja), Mbeya City,Azam FC na Polisi Tanzania aliyopo sasa .

Nchimbi aliwahi kuichezea Mbeya City na  alifanya vizuri kwenye ligi kuu Tanzania na michuano ya FA.

Nchimbi amewahi kuichezea timu ya Njombe mji iliyoshuka daraja msimu wa 2017/18 na Baadae alieachana na timu hiyo.

Post a Comment

0 Comments