advertise with us

ADVERTISE HERE

DIAMOND,MANARA,KITENGE WAWAFUNIKA WACHEZAJI SIMBA NA YANGA KUPIGA PESA

Je unafahamu soka kibongo bongo linalipa kama Ulaya? Kama ulikuwa hujui acha basi leo nikujuze.  Nakuletea mastaa tisa ambao hawajawahi kucheza soka la kulipwa mahali popote lakini wanakula fedha nyingi kuliko wachezaji  wanaozichezea sasa klabu za Simba,Azam na Yanga.

1. HAJI SUNDAY MANARA- MSEMAJI SIMBA
Msemaji na shabiki huyu maarufu  wa Simba hajawahi kucheza ligi yoyote duniani ila anaingiza fedha nyingi sana kupitia matangazo na ubalozi wa makampuni ya  ASAS,AZAMTV na DSTV. Kupitia peji yake ya Instagram Manara amekuwa akiweka matangazo mbali mbali ya makampuni hayo na kujipatia fedha nyingi. Manara amejipatia umaarufu kupitia soka

2. IDRIS  SULTANI- MCHEKESHAJI
Mchekeshaji huyu hana uhusiano wowote na soka ila makampuni mengi makubwa yahusuyo michezo yamekuwa yakimtumia kama balozi wao. Moja ya kampuni hizo ni SportPesa wanaojishugulisha na michezo ya bahati nasibu pia wadhamini wakuu wa Simba na Yanga.

3.  DIAMOND PLATNUMZ - MWANAMUZIKI
Anafahamika kama mwanamziki mashuhuri na mwenye mikataba mingi ya matangazo. Safari hii ameangukia mikonon mwa kampuni inayojihusisha na michezo ya kubahatisha upande wa soka.
Kampuni ya Pari Match imemtumia Diamond kama balozi wa bidhaa zao na wametumia picha za msanii huyo ili kujiongezea umaarufu. Miaka michache iliyopita klabu ya Simba ilimpa nafasi ya kuwa moja ya wageni waalikwa wa tuzo za Mo Simba awards na alilipwa  na  hana historia yoyote katika soka ila

4. SALIMU KIKEKE-MTANGAZAJI WA TELEVISHENI
Wengi tunamfahamu kama mtangazaji wa kituo cha televisheni BBC . amekuwa akitangaza mechi mbalimbali za ligi kuu nchini Uingereza kwa lugha ya kiswahili ila kwa sasa amepata dili kubwa zaidi la kuwa balozi wa klabu ya Simba jijini London Uingereza. Salimu Kikeke hajawahi cheza soka ila anakula fedha za soka kiulaini

5. EDO KUMWEMBE-MTANGAZAJI
Binafsi nimeanza kusoma makala za Edo Kumwembe tangu nikiwa darasa la sita miaka ya 2007. Nilikuwa mmoja wa wanunuaji wa gazeti alilokuwa akilichambua. Edo ni mtu makini sana kwenye soka ingawa hajawahi kucheza soka lakini amelamba dili nyingi zaidi. Kupitia soka edo amelamba dili SuperSport,AzamTv,BinSlum, SportPesa na hata EATV.

6.MAULIDI KITENGE-MTANGAZAJI

Maulid ni shabiki mashuhuri wa klabu ya Yanga na mtangazaji wa kituo cha redio, Jamaa amepata mikataba mingi mikubwa ya kuwa balozi wa makampuni yajihusishayo na soka ingawa yeye hajawahi kuwa mchezaji. Maulidi amepata madili na kampuni za Azam ,SuperSport na Asas .Anakula pesa bila wasiwasi na kiulaini.

7. SHAFII DAUDA-MTANGAZAJI
Unapozungumzia wachambuzi wakongwe hapa Tanzania basi jina la Shafii Dauda haliwezi kukosa. Jamaa ni mbunifu sana na anamiliki vitu mbalimbali kupitia Soka. Shafii amefungua duka la vifaa vya michezo,Online TV ihusuyo michezo pia ni balozi wa makampuni ya Mbet, Startimes na Asas.


8. SALEH JEMBE- MTANGAZAJI 
Salehe Jembe ni moja ya wachambuzi wakongwe wa soka la Tanzania.Anafahamu mengi kuhusu soka la Tanzania ila hajawahi kuwa mchezaji. Jembe anamiliki Blogspot ihusuyo michezo na ni balozi wa makampuni ya SportPesa,Azam Tv,Bin Slum na makampuni mengine . Anapiga hela nyingi kwenye soka na hajawahi kuwa mchezaji.

9. BIN ZUBERY- MTANGAZAJI 
Bin Zubery ni mkongwe zaidi kwenye hii listi na ndio mchambuzi makini sana linapokuja suala la Soka la Tanzania. Bin Zubery hajawahi kuwa mchezaji wa kulipwa ila kupitia soka anaingiza fedha nyingi sana. Bin Zubery anamiliki blogspot na balozi wa bidhaa za Azam,Asas na BinSlum.


Post a Comment

0 Comments