advertise with us

ADVERTISE HERE

TOTENHAM YAPIGWA KIPIGO CHA MBWA KOKO

Klabu ya Tottenham imeshtua mashabiki wa soka baada ya kukubali kipigo kitakatifu toka kwa Bayern Munich. Tottenham iliikaribisha Bayern Munich jijini London kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa ulaya


Dakika ya 12 Son aliipatia BayernMunich goli la kuongoza na Joshua Kimich akarudisha dakika ya 15 kabla ya Lewandowsiky kuwapa bao la pili dakika ya 45, Mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika Bayern Munich 2-1 Tottenham.

Kipindi cha pili dakika ya 53 mchezaji wa zamani wa Arsenal Serge Gnabry aliongeza bao la tatu ,Dakika ya 55 alirejea tena golini . Tottenham walionekana kupoteza mwelekeo kipindi cha pili. Dakika ya 61 walipata penati iliyopigwa na Roy Kane. Gnabry aliwapania Tottenham haswa kwani dakika ya 83 alifunga bao la tatu na Dakika ya 88 akiongeza la nne hukuLewandosk akifunga bao dakika ya 87. Mpira ulimalizika kwa matokeo ya Bayern 7-2  Tottenham.
Kwa matokeo hayo Tottenham inashika nafasi ya 3 kwenye kundi lao ikiwa na pointio 1 na kufungwa mabao 8.

Post a Comment

0 Comments