advertise with us

ADVERTISE HERE

SHAFII DAUDA ALAMBA DILI KUBWA ZAIDI MWAKA

Mchambuzi maarufu wa habari za michezo kupitia redio na televisheni ya Clouds media Bw.Shafii Dauda amelamba shavu kubwa zaidi msimu huu


Meneja Masoko wa Kampuni ya Star Media (T) Limited, David Malisa ameweka bayana kuwa kwenye Chaneli zao za  michezo  kwenye king’amuzi  cha  StarTimes, zimeanza  kuonyesha michuano mikubwa barani Ulaya ya kufuzu Euro 2020 na Europa League.

Mbali na hayo Malisa amesema kwamba kupitia michuano hiyo mtumiaji yeyote wa king’amuzi hicho ataweza kushuhudia mechi kadha wa kadha za timu kubwa za England kama vile Manchester United inayochezewa na Marcus Rashford na Arsenal ya straika Pierre Emerick Aubameyang.


Kupitia michuano hiyo pia Malisa amesema kuwa wamelazimika kuingia kwenye ushirikiano na Mtangaza nguli wa michezo nchini Shaffih Dauda, ambaye atakuwa na jukumu la kuhakikisha anawachambulia baadhi ya michezo wateja wa StarTimes kutokana na uelewa wake katika mambo hayo ya soka.

“Tunafahamu kuwa sehemu kubwa ya Watanzania ni wapenda soka, hivyo kuanzia siku ya Alhamisi (jana), tungependa walipie vifurushi vyao kwani wataanza rasmi kushuhudia mechi kadhaa za Europa League ambapo Shaffih Dauda atakuwa na jukumu la kuchambua na kuwahabarisha baadhi ya mambo yahusuyo soka kupitia mitandao yake ya kijamii lakini hata kupitia StarTimes,” alisema.

Post a Comment

0 Comments