advertise with us

ADVERTISE HERE

MESSI KUREJEA DIMBANI MWEZI NOVEMBA

Mshambuliaji wa Barcelona na timu ya taifa Argentina anategemewa kurejea dimbani hivi karibuni baada ya kufungiwa mwezi august akishiriki Copa America.


Kocha wa Argentina amesisitiza Messi atarejea mwezi Novemba kuitumikia timu yake ya taifa  Argentina 

Messi alifungiwa mechi tatu na shirikisho la soka Amerika Kusini CONMEBOL kwa kugoma kuvaa medali na kusema shirikisho hilo lilipokea rushwa toka kwa Brazil.

Messi alianza kulituhumu shirikisho hilo baada ya kufungwa mabao 3-1 na wenyeji wa mashindano hayo Brazil na baadaye kuifunga Chile kisha kutwaa nafasi ya tatu ya michuano hiyo na Brazil ikinyanyua kombe hilo. 

CONMEBOL ilimfungia Messi na adhabu yake itahitimika mwezi Novemba kisha nahodha huyo kurejea kikosi cha Argentina.

Mbali na Messi kukosekana kwenye mchezo uliochezwa hapo jana dhidi ya Equador timu ya taifa Argentina iliibuka na ushindi wa mabao 6-1.

Post a Comment

0 Comments