advertise with us

ADVERTISE HERE

KOCHA YANGA AWATAJA WALIOIHUJUMU MECHI NA ZESCO

Baada ya kupoteza kwa bao 2-1 dhidi ya Zesco katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika Jumamosi iliyopita, Kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera, amesema endapo angefanya mabadiliko, matokeo yasingekuwa 2-1.


Kocha waYanga, Mwinyi Zahera.
Kauli ya Zahera imekuja kufuatia kutofanya mabadiliko baada ya kuweka wazi kuwa wachezaji wake walikuwa kwenye mipango yake.

Zahera alisema alichelewesha kufanya mabadiliko akiamini mechi ingemalizika kwa sare ya 1-1 na wangeweze kufikia hatua ya kupiga matuta.

Lakini Zahera ameibuka na kusema kama angefanya mabadiliko mapema haswa kuwatoa Abdulaziz Makame na Feisal Salum 'Toto' ambao aliona wamechoka, matokeo yangekuwa mengine.


Fei Toto
"Kama ningefanya mabadiliko mapema ya Toto na Makame waliokuwa wamechoka katika safu ya kiungo ya timu yangu, matokeo yasingekuwa hivyo.

"Nipende tu kuwapongeza wachezaji wangu kwa kupambana vizuri na sasa 
tunaelekeza nguvu zetu zote kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho."

Post a Comment

0 Comments