advertise with us

ADVERTISE HERE

GSM KUMWAGA MAMILIONI ZAID KUIPOTEZA SIMBA

Baada ya kutoa  kiasi cha shilingi za kitanzania milioni 10 katika ushindi wa kwanza wa ligi dhidi ya Coastal Union.




Wadhamini wa klabu hiyo, GSM wameahidi kutoa milioni 50 kwa kila mechi endapo Yanga watapata matokeo, imeelezwa.

Fedha hizo zinawekezwa kwa ajili ya kuzidi kutoa morali kwa timu hiyo ili izidi kufanya vema katika mechi za ligi msimu huu.

GSM wameamua kutoa fedha hizo kutokana namna Yanga ilivyoanza ligi kwa kusuasua na inaelezwa dhumuni la kutoa fedha hizo ni kuhakikisha Yanga inatwaa ubingwa msimu huu.

Milioni 50 hizo zinazidi kutia hamasa ndani ya mabingwa hao wa kihistoria kunako Ligi Kuu maana inaonesha hata wadau, mashabiki, wanachama pamoja na wachezaji wamezifurahia.

Post a Comment

0 Comments