ads

adds

DROGBA NA YEYE KUISHUHUDIA TAIFA STARZ IKIIFUNGA RWANDA

Mara baada ya David Luiz kuwasili nchini Rwanda mchezaji mwingine  mstaafu wa Chelsea na Ivory Coast Didier Droba amewasili nchini humo kwa masuala ya kijamii.



Drogba amewasili Rwanda kwa masuala ya uhamasishaji hasa kwa vijana wa nchi hiyo. Raisi Paul Kagame amekuwa akitumia wanasoka, wanamuziki na hata mastaa wengine ili kuimarisha vijana . Mwezi uliopita alifungua ukumbi mkubwa kwaa jili ya michezo  mbalimbali.


Drogba atafanya kongamano liitwalo Youth Connekt Africa Summit "YCAS 2019". Mbali n hayo nyota hiuyo wa Afrika atautazama mchezo huo.

Drogba ameshakutana na Taifa stars akiwa mchezaji na aliwahi ifunga bao moja pale uwanja wa Taifa  hivyo anaifahamu vyema taifa stazi. Mchezaji pekee aliesalia kwenye timu ya taifa iliyowahi kucheza na Ivory Coast ya Drogba ni Juma Kaseja .


Drogba ataungana na David Luiz kwenye mchezo huo wa kirafiki na wanategemewa kuwa kivutio kikubwa kwa wananchi wa Rwanda.

David Luiz ameshawahi cheza na Didier Drogba na kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Ulaya mwaka 2012.

Post a Comment

0 Comments