advertise with us

ADVERTISE HERE

MTIBWA YAGEUKA KIBONDE LIGI KUU

MTIBWA Sugar,leo inaingia kwenye mtihani mwingine mzito ndani ya Ligi Kuu Bara kwa kucheza na Mbeya City ambayo imetoka kulazimisha sare ya kufungana bao 2-2 na Lipuli FC ya Iringa.

Mpaka sasa kwenye michezo minne imelazimisha sare moja, imepoteza michezo mitatu na ina pointi moja ikiwa nafasi ya 19 jambo linaloongeza presha kwenye mchezo wa leo uwanja wa Jamhuri, Morogoro.

Ofisa Habari wa Mtibwa Sugar, Thobias Kifaru amesema kuwa wamekuwa wakifanyia kazi makosa yao hasa kwenye safu ya ushambuliaji wana imani ya kupata matokeo.

“Tatizo kubwa limekuwa kwenye safu ya ushambuliaji kushindwa kumalizia nafasi ambazo wanazipata ila kwa sasa tuna amini tutafanya vema na kupata matokeo chanya mbele ya wapinzani wetu,” amesema.

Mtibwa Sugar imeikaribisha mara sita Mbeya City Morogoro, imeibuka na ushindi mechi tatu na nyingine tatu waligawana pointi tatu.

Post a Comment

0 Comments