advertise with us

ADVERTISE HERE

MESSI AWEKA REKODI MPYA LIGI YA MABINGWA ULAYA(UEFA)

Lionel Messi ameendelea kuweka historia katika soka baada ya kufunga goli la 100 katika michuano ya Ulaya .
 Lionel Messi mwenye miaka 30 amefikisha rekodi ya magoli 100 baada ya kuifunga Olympiakos. Messi amecheza jumla ya  michezo 122 ya Ulaya. Ronaldo ndiye mchezaji mwenye magoli mengi zaidi 113 na ndiye mchezaji wa kwanza kufikia magoli 100. Lionel Messi alianza kufunga goli la kwanza UEFA dhidi ya Panathinaikos mnamo 2 novemba mwaka 2005 na alifikisha goli lake la 50 uliopigwa tarehe 7 mwezi machi 2012 dhidi ya Bayern Leverkusen akifunga magoli matano peke ake.  Mchezaji mwingine asiye Raia wa Ulaya na amefikisha magoli 50 ni Didier Drogba.

ORODHA YA WACHEZAJI WENYE MAGOLI MENGI ZAIDI UEFA
(N.B alama ya * inamaanisha bado hawajastaafu soka)
113-Cristiano Ronaldo- magoli ( mechi 151*)
100-Lionel Messi (mechi 122*)
76- Raul Gonzalez (158)
70-Philipo Inzaghi (114)
67- Andre Shevchenko (142)
61-Gerd Muller  (69)
59-Thiery Henry (140)
59-Henrick Larson (108)
56-Zlatan Ibrahimovich (139)
54-Eusebio (70)
53-Allesandro Del Piero (129)
51-Karim Benzema (99*)
50-Sergio Aguero (86*)
50-Didier Drogba (102)
50-Klaas-Jan Huntelaar(87*)


Post a Comment

0 Comments