advertise with us

ADVERTISE HERE

IBRAHIM AJIBU AINGIA KATIKA REKODI YA DUNIA

Unaweza usiamini ila ukweli ni kuwa ibrahim Ajibu ameingia katika rekodi ya dunia akijumuika na Ronaldinho, Lionel Messi, Cristiano Ronaldo ,Icard na Marcelo
 Goli la Ajibu dhidi ya Kagera Sugar limemfanya ajibu kuingia katika rekodi ya dunia na kuwa mchezaji wa kwanza Tanzania na Afrika kufanya hivyo.
Wengi wanadhani staili ya Ajibu kuvua jezi ni jambo la kawaida ila tukio hilo linamfanya Ajibu kuwa mchezaji wa kwanza Afrika kushangilia namna hiyo na akiwa mchezaji wa tano duniani kufanya hivyo.
kwa watu wasiofahamu staili ya kuvua jezi haijaanzishwa na Lionel Messi wala  Marcelo wa Real Madrid.bali Ronaldinho aliefanya hivyo mara 2. .
 Mara ya kwanza akiwa nchini Brazil lakini baadaye  akiwa Barcelona katika mchezo dhidi ya Ac milan ligi ya mabingwa ulaya alirudia tena tukio la kuvua jezi. kwa ulaya ndiye mchezaji wa kwanza kufanya hivyo. hawa ni baadhi ya wachezaji wa ulaya waliowahi fanya tukio la namna hiyo
1. MARCELO
 Marcelo alifanya hivyo  mwaka 2014 baada ya kushinda goli katika fainali ya ligi ya mabingwa ulaya dhidi ya Atletico Madrid.
2.LIONEL MESSI
Msimu wa mwaka 2016/17 katika uwanja wa Santiago Bernabeu dhidi ya wenyeji  Real Madrid  Lionel Messi alifunga goli la ushindi  dakika ya 92  kisha kuvua jezi na kuwaonyesha mashabiki. Wengi walidhani staili hiyo ni ya Lionel Messi kuianzisha.

3. CRISTIANO RONALDO

Katika mechi ya Super cup dhidi ya Barcelona uwanja wa Nou Camp Ronaldo alitokea benchi na kufunga kisha alivua shati kushangilia hii ilionekana kulipiza kisasi kwa mpinzani wake Messi lakini yeye aliishia kupata kadi ya njano.
5.ICARDI
Baada ya kuibamiza AC MILAN mabao matatu  Icardi alitoa jezi yake alipokuwa anashangilia.
Ibrahim Ajibu ni mchezaji pekee ligi kuu Tanzania Bara na Afrika kufanya tukio hilo.


Post a Comment

0 Comments