ads

adds

HAZARD AWEKA HISTORIA BAADA YA KUKUTANA NA DONALD DUCK NA KUOMBA PICHA

Kwa mara ya kwanza  nyota wa Chelsea Eden Hazard amefanikiwa kupiga picha na Donald Duck na ameonyesha kufurahishwa na tukio hilo.
Baada ya kufanya vizuri dhidi ya Watford wikiendi iliyopita, Hazard aliamua kwenda nchini ufaransa katika kisiwa cha Disneyland na alipiga picha na moja ya mdoli maarufu duniani ajulikanae kwa jina la Donald Duck. hazard alipost picha akiwa na mdoli huyo na alionyesha kufurahia tukio hilo.
chini ya picha hiyo Hazard aliandika "wiki hii nimekutana na rafiki mpya je wamfahamu".mbali na kwamba Hazard yupo ufaransa Chelsea imeendelea na mzaoezi kujiandaa na michezo inayofuata huku kiungo bora zaidi Ngolo Kante akirejea dimbani na kuanza mazoezi.
Conte anaanza kuwa na amani baada ya tetesi za yeye kutimulia kwa kushidwa kuanza vyema ligi. michezo miwili dhidi ya Everton na Watford imerdisha matumaini mapya kwa kocha huyo na sasa anashikilia nafasi ya nne nyuma ya machester United na Tottenham akizidiwa pointi 4 pekee.

Post a Comment

0 Comments