Subscribe Us

BOLIVIA YAILAZIMISHA SARE BRAZIL

Shukrani za pekee zimwendee kipa wa Bolivia Carlos Lampe kwa kuto ruhusu shuti lolote kupenya langoni mwake dhidi ya Brazil katika kinyang'anyiro cha kufuzu kucheza  kombe dunia 2018 nchini Urusi.
 Mchezo huo ulianza kwa kasi na brazil kuutawala ila walishindwa kupata bao kutokana na uimara wa Lampe golini. timu hizo zilitoshana nguvu kwa 0-0 na Bolivia kuondolewa katika nafasi ya kufuzu michuano hiyo huku Brazil ikiwa imeshafuzu kucheza kombe la Dunia hapo mwakani.
Mchezaji ghali zaidi Neymar alionyesha umahili wake lakini alishindwa kuongeza idadi ya magoli 52 aliyoifungia timu yake ya taifa Brazil.

Post a Comment

0 Comments