advertise with us

ADVERTISE HERE

MANCHESTER UNITED KUMSAJILI SUAREZ

Mchezaji mkongwe wa Manchester United Garry Neville amesisitiza klabu ya Manchester United inatakiwa kumsajili staa Luis Suarez.
 Manchester united imeanza msimu huu vizuri katika michuano yote . upande wa ligi imecheza michezo 6 ikiondoka na point 16 pasipo kufungwa ,ligi ya mabingwa ulaya imecheza michezo miwili ikishinda yote na kombe la ligi EFL imesonga mbele kwa ushindi wa mabao 4 lakini Garry neville ameonekana kuihitaji huduma ya suarez klabuni hapo.
                 Garry Neville amesema Suarez ni aina ya mchezaji anaetakiwa Manchester United
"Hata kama Suarez aliichezea Liverpool ni mchezaji wa manchester united ni vibaya kusema hivyo lakini ni mchezaji mzuri, anafunga magoli na anajituma sana"
Suarez ameichezea Barcelona michezo 110 akifunga magoli 69. kwa upande wa mechi ya ligi ya mabingwa ulaya manchester imeshinda 4-1  dhidi ya cska moscow mbali na kuwakosa wachezaji muhimu kama Paul Pogba, Ibramovich na Marcos Rojo.







Post a Comment

0 Comments