Mchezaji wa Chelsea Tiemoue Bakayoko amepata ajali lakini hajaumia na atakuwepo katika mchezo dhidi ya Stoke city wikiendi hii.
Chelsea ilijikuta ikiingia majaribuni baada ya kiungo wake Tiemoue Bakayoko kupata ajali akitokea mazoezini. Taarifa zinasema kiungo huyo hajapata majeraha yoyote ndani na nje ya mwili.
Gar aina ya mercedes Benz linalomilikiwa na Bakayoko lilivyoacha njia na kuingia porini
Hakuna mtu yeyote aliepata madhara kutokana na ajali hiyo
Kiungo huyo raia wa ufaransa mwenye miaka 23 alijiunga na klabu klabu ya london kwa dau la euro milion 40 na atakuwa klabuni hapo mpaka mwaka 2021.
Kiungo huyo aliekipiga katika klabu ya Rennes kisha kujiunga na Monaco mwaka 2014 amecheza michezo 100 akifunga magoli 5.
Bakayoko ameichezea Chelsea mechio sita akifunga bao moja katika ligi ya mabingwa ulaya dhidi ya Qarabag.
ajali hiyo imetokea muda ambao chelsea imetangaza kumuuza diego costa kwenda Atletico Madrid.
0 Comments