Fabregas amefunguka na kusema Wenger ni kama baba yake , ameyasema hayo wakati akijianda na mchezo wa leo jioni dhidi ya kocha wake huyo aliemkuza.
Cesc Fabregas alilelewa na klabu ya Arsenal na kuwa moja ya wachezaji bora wa klabu hiyo kabla ya kutimkia Barcelona mwaka 2011 kisha 2014 kurejeshwa tena Uingereza na klabu ya Chelsea ingawa alionyesha wazi kutaka kurudiArsenal Fc ila haikuonyesha kumhitaji.
Fabregas atawakaribisha Arsenal darajani katika mchezo wa ligi utakaopigwa saa 3:30 Alasiri jumapili hii.
KIKOSI CHA ARSENAL KITAKACHO ANZA
KIKOSI CHA ARSENAL KITAKACHOANZA
Chelsea FC imecheza michezo minne ya ligi ikifunga magoli 8 kufungwa 5 na pointi 9 huku Arsenal ikishinda michezo 2 na kufungwa 2 kisha kufunga magoli 7 na kufungwa magoli 8. Mchezaji anaetazamwa zaidi ni Alvario Morata akiifungia chelsea magoli matatu.
0 Comments