Diego costa atakipiga katika kwa mkopo klabu ya Al Hilal ya Saudi Arabia endapo dili la kujiunga Atletico Madrid litafanikiwa.Costa alirejea Atletico Madrid na kuilazimisha klabu hiyo imsajili.
Costa alitua jijini madrid akitokea Brazil alikokuwa mapumzikoni, pia costa alizungumza na uongozi wa Chelsea na kuwaeleza hato rejea Darajani mpaka atakapokamilisha kujiunga na Atletico Madrid.
Costa hajashiriki mazoezi na klabu ya chelsea Tangu alipoambiwa hayumo kwenye mipango na kocha wa timu hiyo Anton conte pia ni juzi tu Gari ya Diego costa iliondolewa kwenye paki ya wachezaji kikosi cha kwanza .
Costa alijiunga na chelsea akitokea Atletico Madrid kwa dau la paundi milioni 32 akicheza michezo 109 na kufunga magoli 58 na atarejea Atletico madrid kwa dau la paundi milioni 53.
0 Comments